Mwanasheria wa bingwa wa dunia uzito wa kati anayeshikilia mkanda wa WBO na IBO Mann Pacquiao, Daniel Patroceli amesema anataka kumfikisha mahakamani bondia Floyd Myweather Jr kutokana na bondia huyo pamoja na kambi yake kwa kumshutmu waziwazi bondia wake kuwa anatumia madawa ya kuongeza nguvu na ndio maana alifanikiwa kuwatwanga mabondia wengine kama Oscar De Lahoya na Richard Schaffer.
Mwanasheria huyo amesema kamwe hawezi kuruhusu na kuona bondia wake akirushiwa shutuma hizo.
Bingwa huyo wa dunia amekataa kuchukua vipimo vya mkojo kabla ya mchezo wake na Myweather Jr na yeye mwenyewe anataka kuchukua vipimo hivyo mara baada tu ya mchezo huo ambao umepangwa kuchezwa tarehe kumi na tatu ya mwezi wa tatu