Sunday, January 31, 2010

Misri yafuta machungu ya kukosa kombe la dunia.



Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Misri, Shawaky Gharib amesema timu yake ilicheza vizuri katika michuano ya kombe la mataifa na hadi ikabeba ubingwa kutokana na kuwa na machungu ya kukosa nafasi ya kucheza kombe la dunia nchini Afrika Kusini.


Kocha huyo ameongeza na kusema kombe la mwaka huu lilikuwa gumu kutokana na timu hiyo kukumbana na mataifa ambayo yatashiriki katika fainali za dunia.


kwa upande wake, mlinda mlango wa Misri Essam El Hadary amesema kikosi chake ndicho kikosi bora katika wakati huu.

Fergie akisifu kikosi chake kwa kuilaza chali Arsenal


kocha mkuu wa klabu ya manchester united, sir alex fergusson amekisifu kikosi chake kwa kuonesha kandanda safi hapo jana na kufanikiwa kuichabanga klabu ya Arsenal goli tatu kwa moja.


Fergie amesifu mbinu aliyoitumia ya kushambulia kwa kushtukiza ambayo iliisaidia kwa kiasi kikubwa timu yake dhidi ya arsenal iliyokuwa imetawala mchezo pamoja na kuishambulia man united mara kwa mara.

Kwa upande wake kocha wa klabu ya Arsenal, Arsen Wenger amekiri kuwa kikosi chake kilicheza mchezo mbovu na makosa ya mchezaji mmoja mmoja yaliigharimu timu yake

Dimba la emirates lipo tayari kwa arsenal na man u



Timu ya taifa ya Togo imefungiwa kushiriki michuano miwili ijayo ya kombe la mataifa ya afrika pamoja na kupigwa faini ya dola elfu hamsini kutokana na kujiondoa katika michuano hiyo inaomalizika leo huko Luanda Angola.


Caf imesema imeamua kutoa adhabu hiyo kutokana na serikali ya Togo kuwashinikiza wachezaji wajiondoe huku wachezaji hao wakitaka kucheza michuano hiyo.


Nayo serikali ya Togo imejibu mapigo na kuishutumu CAF kwa kutoa adhabu hiyo ambapo waziri wa mambo ya ndani ya Togo Paschal Bodjona amekarirwa akishangazwa na uamuzi huo huku akisema Caf haijali maisha ya watu waliopotea maisha wakati timu hiyo iliposhambuliwa na waasi huko Cabinda.


Togo ilishambuliwa na waasi wa Cabinda tarehe nane ya mwezi wa pili ambapo katika shambulio hilo maofisa wawili waliwawa

Terry akumbwa na kashfa ya mapenzi




Nahodha wa timu ya taifa ya uingereza na klabu ya Chelsea ya uingereza, John Terry anakabiliwa na kashfa kubwa ya kumpa mimba mpenzi wa mchezaji mwenzake wa zamani Wayne Bridge.
Inasemekana kuwa Terry alikuwa anatembea na mpenzi huyo wa bridge anayejulikana kwa jina la Vannesa ambaye ni mwanamitindo kutoka nchini Ufaransa. Katika habari za ndani zaidi zinaeleza kuwa Vannesa ametoa mimba hiyo aliyopewa na terry miezi michache iliyopita.

Terry anayepokea kitita cha paund laki moja na sabini kwa wiki alianza mapenzi na vannesa mara baada ya wayne bridge kuuzwa kwa klabu ya Manchester City mwezi wa kwanza mwaka jana

Friday, January 29, 2010

Thursday, January 28, 2010

Misri na Ghana Fainali jpili




Misri imeichapa Algeria iliyomaliza ikiwa na wachezaji nane goli nne kwa buyu katika mchezo wa nusu fainali na kufanikiwa kutinga fainai pamoja na kulipiza kisasi cha kufungwa na mahasimu wake hao wa jadi katika ukanda wa kaskazini mwa Afrika.
Katika mchezo wa mapema, Ghana iliichapa Nigeria goli moja kwa bila na hivyo kufanikiwa kuingia fainali ambapo sasa itacheza na Misri.

Goli la Ghana lilifungwa na Asamoah Gyan ambaye baaada ya filimbi ya mwisho aliangua kilio na alipohojiwa kulikoni alikiri kuwa hakuamini kama kikosi kilichosheheni wachezaji wachanga kama hao kingeweza kufika katika hatua hiyo.

Kama Misri chini ya kocha wake mkuu Hassan Shehata ikichukua ubingwa basi itakuwa imeweka rekodi ya kukibeba kikombe hicho mara saba.

Spotidesk inapochana mawimbi


Murray atinga fainali


Mcheza tennis Andy Murray amefanikiwa kutinga katika hatua ya fainali ya mashindano ya wazi ya Australia baada ya kumshinda Marin Cilic kwa seti 3-6 6-4 6-4 6-2 katika mchezo uliochezwa kwa masaa matatu.


Kwa matokeo hayo Murray atacheza na mshindi kati ya Federer na Tsonga katika fainali ya mashindano ya wazi ya Australia ambapo mchezo wa fainali utachezwa jumapili.

Yanga yatamba kuifunga Majimaji jmosi




Mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Yanga wametamba kufanya vizuri katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Majimaji licha ya kuwakosa wachezaji wake muhimu watatu, Mrisho Ngasa na Abdi Kassim kutokana na majeruhi huku Nurdin Bakari akiwa na anakabiliwa na kadi mbili za njano.


Katika hatua nyingine kocha mkuu wa klabu hiyo Kostadin Papic amesema itakuwa ni vigumu kwa timu yake kucheza michezo ya kimataifa ya majaribio nje ya nchi kutokana na kubanwa na muda wa kujiandaa kucheza na klabu ya Lupopo ya kutoka DRC ukiwa mchezo wa ligi ya mabingwa wa Afrika.

Tuesday, January 26, 2010

Sauti za Busara kuanza kusikika trh 11 FEB




Tamasha la saba la sauti za busara linatarajia kuanza kufanyika kuanzia tarehe kumi na moa ya mwezi huu mpaka tarehe kumi na sita katika uwanja wa ngome kongwe uliopo stone town, Zanzibar.


Mwenyekiti wa tamasha hilo ambaye pia ni kiongozi wa bendi ya kilimanjaro, Waziri Ally amesema wana imani kuwa tamasha la mwaka huu litafana kwa kuna wasanii wakubwa kutoka nchi ya zambia, guinea, afrika kusini, marekani na mataifa mengine watatumbuiza.


Kwa upande wake msanii fresh jumbe anayefanya shughuli zake nchini Japan amesema anaimani tamasha la kumi la busara litakuwa bora zaidi kuliko matamasha yote Afrika.

Robinho kuichezea Santos kwa mkopo


klabu ya manchester city ya uingereza imethibitisha kutaka kumtoa kwa mkopo mshambuliaji wake iliyemnunua kwa bei ghal kutoka real madrid Robinho.

kocha mkuu wa City Roberto Mancini amekaririwa akisema kuwa city inafanya mazungumzo ya mwisho mwisho na Santos ili mchezaji huyo ahamie katika klabu yake hiyo ya zamani.

Mancini ameongeza na kusema kuwa anataka kumsaidia robinho aende sehemu ambayo atacheza mara kwa mara ili aweze kupata namba katika kikosi cha timu ya taifa ya brazil kitakachoshiriki katika fainali za kombe la dunia nchini afrika kusini.

Monday, January 25, 2010

Jua alikuchi nusu fainaliAFCON

Wapinzani wa jadi ambao siku zote hawapikiki chungu kimoja wanatarajia kuchuana katika nusu fainali zote mbili za kombe la mataifa ya Afrika. Wapinzani wa kaskazini mwa Afrika Ageria almaarufu kama mbwa mwitu wa jangwani watakabiliana na Mapharao wa Misri ambao watakuwa na mawili kichwani la kwanza kupata ushindi na kutinga fainali huku la pili likiwa la kulipiza kisasi cha kuondoshwa katika fainali za dunia na mbweha hao wanaocheza kwa kasi dakika zote za uwanjani.

Wakati mambo yakiwa hivyo katika nusu fainali hiyo inayokutanisha miamba ya kaskazini, huko magharibi ya afrika kutakuwa na patashika nguo kuchanika kwa kukukutanisha timu ya taifa ya Nigeria almaarufu kama tai mwenye nguvu atakuwa anakabiliana na Ghana nyota weusi mchezo ambao untarajiwa kuwa wa vute ni kuvute kutokana na upinzani uliopo baina ya miamba hiyo ya afrika magharibi

JABULANI WAWA GUMZO AFCON




Mpira utakaotumika katika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Afrika kusini JABULANI umekuwa gumzo katika fainali za mataifa ya afrika kutokana na kasi yake pindi unapopigwa.

Tayari baadhi ya walinda walango wameshatoa kilio chao kuhusiana na mpira huo wenye jina la kizulu ambalo linamaanisha shangwe kwa lugha ya kiswahili.

Kampuni ya adidas inayotengeneza vifaa vya michezo imekuwa na kawaida ya kutoa aina tofauti ya mipira kila inapofika katika fainali za dunia.




Soka letu lipo enzi za UJIMA!




Hivi ni mimi tu au hata wewe unafikiri hili, mi naona bado soka letu lipo katika UJIMA, embu angalia biashara za karanga, maji ya kunywa, barafu na vitu kede kede vikiuzwa bila mpangilio, hapo bado kitu kibao cha kuonesha matokeo ni vibati tu vimechokaa alafu vya kitambo next time nitakuonesha picha zake ili uweze kuungana na mimi kuwa soka letu lipo enzi za ujima.

Yanga kutumia michezo ya ligi kujiwinda na Lupopo







Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Yanga imesema inatumia michezo ya ligi kuu ya Tanzania Bara kama kipimo ama maandalizi ya kujiandaa na mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi ya mabingwa wa afrika dhidi ya Lupopo kutoka DRC.

Akizungumza katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya timu yake na Manyema, Afisa Habari wa klabu hiyo Luis Sendeu amesema kuwa licha ya kutumia michezo ya ligi kama maandalizi ya kuivaa lupopo lakini pia inataraji kucheza na klabu ya URA kutoka Uganda pamoja na klabu moja kutoka kenya.

Katika mchezo wa jana, Yanga iliichabanga Manyema goli tatu kwa moja magoli ya Yanga yakifungwa na Mrisho Ngasa huku la Manyema likifungwa na Ally Mohamed.

Saturday, January 23, 2010

Rooney aishusha Arsenal kileleni


Magoli matatu yaliyofungwa na wayne rooney yametosha kuishusha Arsenal kileleni mwa ligi kuu ya Uingereza, minachosubiriwa sasa ni mtanange baina ya wakali hao mh mi naakaa kimya sjui nani atakuwa mbabe

mjomba vipi tena! unahitaji msaada?


Simba ya tafuna maafande uhuru




Klabu ya simba imeendelea na kasi yake ya kusaka ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa timu ya Tz Prisons kwa goli tatu kwa moja katika uwanja wa Uhuru. Magoli ya simba yamefungwa na Mussa Hassan Mgosi mawili dakika ya 2 na 56 huku Nicholas Nyagawa akipachika jengine dakika ya 16 na lile la prisons lilipatikana katika kipindi cha pili dakika ya 62.

Uchaguzi mkuu simba mwezi wa tano


Uchaguzi mkuu wa klabu ya simba unatarajiwa kufanyika tarehe tisa ya mwezi wa tano mwaka huu. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi wa klabu hiyo, Salum Madenge amesema kuwa uchaguzi huo utafanyika tarehe hiyo katika eneo ambalo litapangwa hapo baadae na kamati ya utendaji

Friday, January 22, 2010

RT yajitoa katika matumizi ya uwanja mpya kwa timu ya riadha


RT
Chama cha riadha nchini kimesema hakihusiki na utoaji wa ruhusa wa matumizi ya uwanja wa taifa kwa wachezaji wa timu ya taifa ya riadha inayofanya mazoezi katika uwanja wa uhuru kujiandaa na michezo ya jumuiya ya madola yatakayofanyika hapo baadae katika jiji la New Delhi nchini India.

Akiongea na redio Mlimani, katibu mkuu wa RT, Selemani Nyambui amesema, wizara ya habari, utamaduni na michezo ndiyo inadhamana ya kutoa ruhusu kwa timu hiyo kufanyia mazoezi yao katika uwanja huo wenye sifa na viwango vyote vya olimpic.

Hapo awali, dawati la michezo la redio mlimani lilitembelea katika kambi ya timu ya taifa ya riadha na kuonana na kocha wake mkuu Adrew Baro ambaye alieleza bayana kuwa timu yake inakabiliwa na mazingira magumu yakufanyia mazoezi katika uwanja wa uhuru kwakua uwanja huo hauna sifa zozote za mchezo wa riadha.

Kocha huyo raia wa Cuba ameongeza na kusema kuwa, wameshapeleka barua wizarani ya kuomba kupaiwa uwanja huo japo mara mbili kwa wiki lakini hadi sasa jitihada zao zimegonga mwamba na hawaelewi nini tatizo.

Mwishoni mwa mwaka jana wakati wa hafla ya kupokea kifimbo cha malkia cha michezo ya jumuiya ya madola, Rais Jakaya Kikwete ambae ni mdau mkubwa wa michezo aliweka bayana kuwa dhamira ya serikali yake kwa sasa ni kuuinua mchezo wa riadha ambao katika miaka ya hivi karibuni umedorora tofauti na miaka ya nyuma.

Kobe aweka rekodi NBA


NBA
Mchezaji nyota wa kikapu anayechezea kabu ya Los Angeles Lakers inayoshiriki ligi ya mpira wa kikapu nchini Marekani, NBA, Kobe Brayant amekua mchezaji wa ishirini na tano kufikisha point 25,000

Bryant mwenye umri a miaka 31 amefanikiwa kuingia katika rekodi hiyo katika mchezo ulioikutanisha timu yake na Cleveland Cavaliers ikiwa ni siku thelathini na tano baada ya nyota mwingine wa mpira wa kikapu nchini humu Wilt Chamberlain kustaafu kucheza akiwa amefunga jumla ya vikapu 31,419.

Katika orodha hiyo ya wachezaji ishirini na tano, wacheaji wanaomfuatia kwa karibu ni Jerry West ambaye amefikisha vikapu 25192 na mchezaji wa zamani wa Indiana Pacers Guard Reggie Miller ambaye amefikisha vikapu 25279.

Kinara anayeongoza katika orodha hiyo ni Kareem-Abdul-Jabbar ambaye anarekodi ya kufunga vkapu 38,387

Tevez amuita Neville mgonjwa wa akili



Mshambuliaji hatari wa klabu ya Manchester City na timu ya taifa ya Argentina, Carlos Tevez amemuita mlinzi na nahodha wa watani wao wajadi Manchester United, Gary Neville mgonjwa wa akili wakati akielezea sababu zilizomfanya ashangilie kwa kwa kumkebehi mlinzi huyo mkongwe.

Tevez ameongeza na kusema kuwa, aliamua kufanya hivyo hasa kutokana na Neville siku moja kabla ya pambano la nusu fainali na Man u, alikaririwa akisema kuwa tevez hakustahili kuuzwa kwa paund million 25 kwa kuwa hana kiwango cha kuuzwa bei hiyo.

Tayari chama cha soka nchini uingereza kimevitaka klabu hizo mbili za jiji la Manchester kucheza kwa nidhamu katika mchezo wa marudiano utakaochezwa katika dimba la Old Trafford wki ijayo.

CAF: Zambia ndio vinara wa kundi D


Timu ya taifa ya Zambia itachuana na timu ya taifa Nigeria katika mchezo wa robo fainali wa kombe la mataifa ya afrika utakaochezwa wiki ijayo.


Kwa mujibu wa taarifa ya CAF, zambia ndio vinara wa kundi D kutokana na kuwa na idadi kubwa ya magoli kuliko Cameroun na Zambia kwa mantiki hiyo itakabiliana na mshindi wa wapili wa kundi C ambaye ni Nigeria huku Cameroun wakichuana vikali na mabingwa watetezi wa kundi hilo Misri.


Mara baada ya mtanange kumalizika kati ya Zambia na Gabon, kocha mkuu wa Misri Hassan Shehata alionekana akifurahia lakini ilishindwa kufahamika kamaalikuwa na furaha ya kukutana na Cameroun au la!


Matokeo ya kundi D yamewachanganya sana mashabiki wa soka kutokana na Zambia na Cameroun kuwiana kwa point pamoja na magoli yakufunga na yakufugwa.

Tuesday, January 19, 2010

Mancini kicheko, Fergie ajipa moyo, Tevez Shangwe







Kocha mkuu wa klabu ya Manchester City, Roberto Mancini amewapongeza wachezaji wake kwa kucheza kwa kujituma na kufanikiwa kuwachabanga wapinzani wake wa jadi klabu ya Manchester united katika nusu fainali ya kombe la ligi, Carling Cup.

Mancini amempongeza mshambuliaji machachari wa City, Carlos Tevez kwa kucheza vizuri na kufanikiwa kupachiaka wavuni magoli mawili lakini ameongeza na kusema kuwa kitu muhimu ni kuona timu nzima ilicheza mchezo mzuri.

Akizungumzia mchezo wa marudiano ambao utachezwa jumatano ijayo, Mancini amesema kuwa timu yake itaingia uwanjani ikiwa mbele kwa goli mbili dhdi ya moja lakini bado anaamini mchezo huo utakuwa ni mgumu.

Kwa upande wake kocha mkuu wa Manchester United, Sir Alex Fergusson amesema litakuwa ni jambo la kijinga kudhani kuwa timu yake imeshatolewa katika kombe hilo na bado anamini timu yake itafanya vizuri katika mchezo wa marudiano kutokana na kutawala sehemu kubwa ya mchezo huo.

Heka heka ya usajili Ulaya




Klabu za soka barani ulaya zimeendelea na heka heka ya kusajili wachezaji katika dirisha dogo la usajili huku pia zikiwa n mipango ya kusajili wachezaji wengine.


Kocha mkuu wa klabu ya Totenham Hotspurs Harry Redknap ameonesha nia ya kutaka kumsajili mshambuliaji mkongwe raia wa udachi, Rud Van Nesteroy kutoka klabu ya real Madrid lakini anaweza akafanya hivyo endapo atafanikiwa kumuuza mshambuliaji wa Urusi Roman Pulvuchenko.


Nayo klabu ya Middlesbrough inampango wa kumsajili jamal Campbell kutoka katika klabu ya ligi daraja la kwanza nchini humu BarnsleyWakala wa kiungo wa Liverpool na timu a taifa ya Italia Alberto Aquilani anaona kioja habari zinazomuhusisha mteja wake na kujiunga na miamba ya serie A Juventus ktika dirisha dogo la usajili

Monday, January 18, 2010

Azam yalazimishwa sare na Kagera Sugar







Klabu ya Azam imelazimishwa sare na Kagera sugar ya goli moja kwa moja katika mchezo uliochezwa jioni ya leo katika dimba la taifa, alikuwa ni kiraka mkogwe said sued aliyepachika goli la kwanza kwa upande wa Azam baada ya kupiga shuti kali kwa mpira wa adhabu ambalo lilimzidi mlinda mlango wa Kagera Sugar Amani Simba.

Goli hilo almanusuru livuruge mchezo huo kutokana na wachezaji wa Kagera Sugar kumzonga mwamuzi huyo na kudai kuwa mpira haukuvuka mstari wa golini.

Kufuatia goli hilo, Kagera Sugar walichachama na kusawazisha katika dakika ya tisini kupitia kwa Said Dilunga.

Ligi hiyo itaendelea tena hapo kesho kwa mchezo dhidi ya Moro United na Tanzania Prisons.

TBF yahaha kumbakiza kocha wa ngumi




Shirikisho la ngumi za ridhaa nchini, TBF limesema litahakikisha kila liwezekanalo kumbakisha kocha wa timu ya taifa Giov anis Hurtado ambaye imeripotiwa kuwa anataka kuondoka kutokana na mazingiraz magumu anayokabiliana nayo katika kufundisha kikosi hicho.

Kauli hiyo imetolewa na katibu mkuu wa TBF, Makore Mashaga wakati wa mazoezi ya timu ya taifa yanayofanyika katika uwanja wa ndani wa taifa.

Kutokana na hali mazingira magumu yanayoikabili kambi ya timu ya taifa ya ngumi za ridhaa ikiwemo kukosa vifaa muhimu vya mazoezi imedaiwa kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya ngumi za ridhaa, Giovanis Hurtado ana mpango wa kuacha kazi na kurudi kwao CUBA.



Kutokana na hio, Katibu Mkuu wa TBF Makore Mashaga anaweka bayana jitihada za shirikisho lake la kupata ufumbuzi wa matatizo ya kamb pamoja na kocha huyo.


Timu ya taifa ya ngumi za ridhaa nchini inatarajia kuelekea nchini India katika mashindano ya maandalizi ya michezo ya jumuiya ya madola yanayotarajia kuanza mwezi wa kumi.

Wakati huo huo, bingwa wa dunia wa uzito wa kati anayeshikilia mkanda wa ICB na WBC, Francis Cheka amelitaka shirikisho la ngumi za kulipwa nchini TPBO pamoja na PST kumtafutia mapambano makali ili uwezo wake uzidi kuongezeka.


Cheka baada ya kumchapa Isack Tevez na kuchuka mkanda wa WBC anatarajia kupanda ulingoni mwezi wa tatu mwaka huu ambapo anatarajia kuchuana vikali na bondia kutoka nchini afrika kusini lakini hadi sasa bado ajatambulika ni nani.

Sunday, January 17, 2010

Serena yupo fiti kutete taji lake la AUS


Bingwa wa michuno ya wazi ya tennis ya Australia, Serena Williams amesema yupo fiti kutetea taji lake hilo licha ya kuonekana akiwa anachechemea katika mchezo wake wa fainali wa mashindano ya Sdney dhidi ya Elena Dementiev ambapo serena alipoteza mchezo huo.

Akizungumzia hali ya goti lake serena amesema kuwa, kwasasa goti lake limepona kabisa na anataka adhihirishe hilo kwa kucheza kwa kiwango cha juu katika mashindano hayo ambao ataanza kwa kucheza na mchezaji kutoka Poland Urszula Radwanska jummanne ya wiki ijayo na kama atatwaa tena kikombe hicho basi itakuwa ni mara ya tano kwake kuwa bingwa wa michuano hiyo ya wazi ya Australia.

Zambia uso kwa uso na Simba, Gabon yasaka ushindi




Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Zambia herve renard amewataka wachezaji wake kucheza kwa umakini mkubwa katika mchezo wa usiku wa leo dhidi ya Cmeroun kwakuwa siku zote simba aliyejeruhiwa huwa ni mkali zaidi.

Kocha huyo ambaye ndiye kocha kijana kuliko makocha wote katika kombe la mataifa ya afrika amesema haihofii cameroun katika mchezo wa leo lakini anaaamini timu hiyo haitorudisha makali yake yanayoonekana kuwa butu kwao huku akisisitiza kuwa anaamini timu yake itawaondosha mabingwa hao wa mara nne wa bara la afrika lakini ametaka watu wachukulie mchezo wa leo kuwa ni kati ya Zambia na Cameroun na wala sio vita kati ya makocha wawili wa ufaransa.

Zambia almaarufu kama Chipolopolo itashuka kucheza na simba hao wasiofugika wakiwa na kumbukumbu nzuri ya kupata kichapo cha goli tano kwa moja kwenye fainali zilizopita zilizochezwa nchini Ghana mwaka 2008.

Wakati mambo yakiwa hivyo Kwa Zambia na Cameroun, timu ya tafa ya Gabon almaarufu kama Azengo itakuwa na kazi ya ziada itakapokuwa inavaana na timu ya taifa ya Tunisia ambao wanajulikana kwa jina la Tai wa jangwani.
Gabon inahitaji ushindi tu hii leo ili kujihakikishia nafasi ya kuingia hatua ya robo fainali ya mashindano hayo baada ya kuicharaza Cameroun kwa goli moja bila katiaka mchezo wa kwanza goli lililofungwa na Cousin ambaye anakiputa katika klabu ya Hull City ya nchini Uingereza.

Jumbe arudi nyumbani


BENDI kongwe ya muziki wa Dansi nchini ya Msondo Music imemludisha kundini mwimbaji wake maili, Huseni Jumbe 'Mzee wa Dodo' baada ya kukaa nje ya bendi hiyo kwa mwaka mzima

Akizungumza Dar es Salaam jana, Msemaji wa kundi hilo, Rajabu Mhamila 'Super D'Alisema, wameamua kumrudisha kundini mwimbaji huyo baada ya kukaa viongozi na kukubariana nae na sasa ameshaanza kupanda katika jukwaa la bendi hiyo ambapo mpaka sasa tunajipanga kutoa nyimbo mpya za mwaka uhu baada ya mwaka jana kutambulisha albamu yetu ya huna shukrani na kuwa ipo mtaani kwa sasa inauzwa,

Wakati huohuo, bendi hiyo kwa sasa imekuwa ikitoa burudani za wazi katika kuwaweka karibu wapenzi wake ambapo kila jumamosi tunakuwa katika viwanja vya TCC Chan'gombe na jumapiri uwa tupo Leaders Club jijini Dar es Salaam

Alisema, sambamba na burudani hizo pia wamejipanga kutoa nyimbo mpya kila baada ya wiki tatu ili kukamilisha albamu ya mwaka uhu mapema kadri iwezekanavyo alisema Mhamila,
Akitoa wito kwa wapenzi wa bendi hiyo kuhudhulia kuona maonesho yao popote yafanyikapo kwani kuna burudani ambazo azihitaji kuadithiwa

Saturday, January 16, 2010

Yanga na African Lyion jioni leo




Pazia la ligi kuu ya Tz Bara linafunguliwa hii leo kwa mchezo mmoja ambao utawakutaniasha mabingwa watetezi wa kombe hilo dhidi ya African lyion katika dimba la uhuru.


Mchezo huo unatarajia kuwa mzuri na ushindani kutokana na maandalizi ya kila timu, Yanga ambayo sasa inanolewa na Kostadin Papic imeonekana kubadilika vya kutosha ukilinganisha na mzunguko wa kwanza huku African Lyion ikimchukua Charles Boniface Mkwasa ´Master´ na kuwachukua kwa mkopo wachezaji Meshack Abel, Adam Kigwande pamoja na kumsajili mlinda mlango wa zamani wa Yanga, Ivo Mapunda.


Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza, Yanga ilikwenda sare na vijana hao wa Temeke.

Friday, January 15, 2010

Mrithi wa Maximo aanzwa kutafutwa


Mchakato wa kumtafuta kocha mpya wa timu ya taifa, Taifa stars umeshanza ambapo kamati inayongozwa na katibu mkuu wa shirikisho hilo Fedrick Mwakalebela imesema sifa za kocha anayestahili kumrithi mbrazil huyo zitawekwa bayana wiki ijayo.


Katika hatua nyingine, Mwakalebela ameongeza kuwa si kweli kwamba TFF haina mpango wa kuajiri kocha mzawa kama habari zilivyoenea kuwa shirikisho hilo la soka halinampango wa kuajiri kocha mzalendo.


Hadi hivi sasa, TFF imeshapokea maombi ya makocha kutoka, Mexico, Uingereza, Ufaransa na Tanzania.


Mkataba wa Maximo unamalizika mwezi wa sita mwaka huu.

Ndege inayopaaaaa nchi kavu!