Thursday, May 6, 2010

Maurinho aipa Inter kombe la kwanza




Alikuwa ni Diego Milito aliyewanyamazisha mashabiki wa AS Roma katika dimba la Olimpico na akiwainua mashabiki wa milan waliokuwa wachache uwanjani lakini wengi katika jiji la Milan kushangilia kombe lao la kwanza msimu huu huku wakiyasubiria mengine mawili.

Aliyekuwa na furaha zaidi ni Jose Maurinho ambaye baada ya kuifunga Roma goli moja kwa bila katika mchezo huo wa kombe la ligi la italia, amesema hatimaye ndoto yao ya kwanza imetimia

Inter hivi sasa inapigana kuchukua kombe la ligi kuu ya nchi hiyo pamoja na ligi ya mabingwa barani ulaya.

No comments:

Post a Comment