Wednesday, May 5, 2010

Redknapp: Pressure ipo kwa Man city sio sisi




Kocha mkuu wa klabu ya totenham hotspurs, harry redknapp amesema presha kwa sasa ipo kwa man city na sio kwa klabu yake,.

redknapp moja ya makocha wanaoheshimika sana nchini uingereza ametoa kauli hiyo kabla ya miamba hiyo miwili kuvaana usiku wa leo katika mchezo unaoweza ukaamua ni nani atamaliza katika nafasi ya nne na hatimaye kushiriki katika michuano ya ligi ya mabingwa ulaya.

Kocha huyo wa zamani wa klabu ya portsmouth amesema kuwa wakati ligi inaanza watu wengi waliipigia chapuo man city kumaliza ya nne hivyo anaamini wapinzani wao watashuka dimbani kwa kupania ili watmize adhma yao lakini huku wakihofi timu yake kushinda kwani kama ikishinda leo itakuwa imejihakikishia kabisa kucheza ligi ya mabingwa ulaya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment