Wednesday, May 5, 2010

Mourinho: Nipeni heshima yangu


Kocha mkuu wa InterMilan Jose Maurinho amewataka mashabiki wa InterMilan kumpa heshima yake kutokana na kuisaidia klabu hiyo kufika katika fainali ya mabingwa barani ulaya, kombe la italia na sasa timu hiyo inafukuzia taji la ubingwa wa ligi la nchi hiyo.

Kocha huyo raia wa ureno anaamini timu yake ina nafasi ya kubebwa kikombe cha italia hii leo wakati timu yake itakapokuwa ikivaana na AS Roma katika dimba la olimpico.

akiuzungumzia kikosi chake kabla ya mchezo huo, maurinho anasikitishwa kwa kumkosa kiungo wake mahiri Sjneider pamoja na mlinzi wake mahiri kutoka brazil Lucio lakini bado anaamini atafanya vizuri katika mchezo huo.

Alipoulizwa kuhusiana na nini anachokikumbuka tarehe tano ya mwezi wa tano, kocha hyo mwenye visanga vingi amesema anachokumbuka ni kifo cha Napoleone Bonapatre.

No comments:

Post a Comment